Siku mdau wako alipotembelea hifadhi ya Manyara kufanya utalii wa ndani



 

DSCN5278Mapokezi ambapo kuna ramani ya hifadhi yote. Hapa ni mtu yeyeote anaruhusiwa kutembelea bure na kujionea baadhi ya vivutio viachache vilivyohifadhiwa.

DSC00242Kwa mbali wanaonekana wanyama aina ya Kiboko wamepumzika

DSC00221Shughuli za utalii katika hifahdi hii hufanywa zaidi na magari ya aina hii ambayo ayanaelezwa kuwa na uwezo mzuri wa kuhimili mikikimikiki ya njia za vumbi

DSC00223Hiki ni kinyesi cha tembo, baadhi ya watu wanadai kinaweza kutumika kama dawa kwa namna mbalimbali

DSC00235Msafara wa tembo na vitoto vyao vikikatiza katikati ya tulipopaki magari. Kuna waliocheka kuna waliokaribia kulia na wengine kutaka kukimbia wakati tembo hao wakititisha mikonga yao jirani kabisa na kioo cha gari. Mhudumu alitufahamisha kuwa unapokuwa nadani ya hifadhi unapaswa kuwa na heshima na kuzingatia maelekezo yaote ya usalama. Kwa mfano, tembo kama hawa wakiwa wanazunguka gari yako, huna haja ya kuogopa…unatulia tu na kuacha wamalize shughuli yao. Tour Guider alituambia kuwa ni makosa makubwa sana kuwasha injini ya gari ikitokea hali ya namna hii au kujaribu kuondoa gari kwa nguvu.

DSC00265Mapumziko baada ya mizunguko ndani ya hifadhi

DSC00285Hapa ni mahali yanapatikana maji ya moto moja kwa moja toka ardhini. Maji Moto na Bonde la Ufa katika hifadhi ya Ziwa Manyara

DSC00300Mwenzetu katika msafara, Festo Tarimo akijaribu kuhakikisha kama maji hayo yanamoto kweli…

DSCN5284Kabla ya kuanza ziara ndani ya hifadhi ya Manyara

DSCN5305Kuna baadhi ya wanyama huwa ni adimu sana kuwaona maana mara nyingi huwahi kukimbia. Hapa tulibahatisha kuwaona wanyama aina ya Ngiri wamejichanganya na wanyama sampuli nyingine!

Posted by SeriaJr on Friday, October 12, 2012 0 Maoni yako?

Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Taswira Mtaani: Mafunzo ya Mgambo

DSCN5723Vijana wa Jijini Arusha walio katika mafunzo ya askari mgambo wakitembea “kikakamavu” kama walivyokuta na camera yetu muda mfupi uliopita katika barabara ya Old Moshi. Makampuni mengi ya ulinzi yamekuwa yakiwatumia vijana hawa baada ya kumaliza mafunzo kwa ajili ya shughuli za ulinzi katika majumba ya watu, maofisi, karakana au viwanda na hivyo kusaidia tatizo la ajira kwa kiasi fulani.



Responses

0 Respones to "Siku mdau wako alipotembelea hifadhi ya Manyara kufanya utalii wa ndani"

Post a Comment

 

Recent Comments

Popular Posts

Return to top of page Copyright © 2010 | Platinum Theme Converted into Blogger Template by HackTutors